
Monetize Telegram Mini App with Telega.io
Connect your app, set CPM, and watch your revenue grow!
Start monetizing
22.6

Advertising on the Telegram channel «HADITHI TAMU ZA MAPENZI❤️»
5.0
Books, Audiobooks & Podcasts
Language:
English
267
0
Share
Add to favorite
Buy advertising in this channel
Placement Format:
keyboard_arrow_down
- 1/24
- 2/48
- 3/72
- Native
- 7 days
- Forwards
1 hour in the top / 24 hours in the feed
Quantity
%keyboard_arrow_down
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 8
- 10
- 15
Advertising publication cost
local_activity
$7.20$7.20local_mall
0.0%
Remaining at this price:0
Recent Channel Posts
"Amina weee japo sijasomea mapishi lakini kitu pekee anacho angalia mlaji wa aina yoyote yule ni ladha...."
"Ladha?...."
"Ndiyo, kuna namna moyo wangu unaniambia huu ndio wakati wako wa kufanikiwa" Mamkubwa aliongea kisha akaingia ndani, sikuelewa maana ya maneno yake
Kazi ya mgahawa inachosha hatari, Mamkubwa alifunga mgahawa wake saa nne kamili usiku.
Nilifika nyumbani nikiwa nimechoka sana, sikuwa na ratiba ya kuoga nililala hivyo hivyo.
Simu yangu ilianza kuita, niliichungulia kwa jicho moja. Ilikuwa ni namba mpya sikuwa tayari kuanza kujieleza.
Mpigaji alionekana kuwa mkorofi sana, niliamua kuizima simu kisha ni kalala.
Kulivyo pambazuka asubuhi niliitwa kwenda kuamua ndoa ya jirani yangu.....kuna namna naaminika sana katika mtaa wa Igogo B, kuna muda najionaga kama hakimu hivi. Hata bila kunawa uso wenye kesi walionekana kunivumilia tu.
Nilitumia masaa 4 kutatua kesi ya Wanandoa, niliachia tabasamu baada ya kuona nimeeleweka.
Nilirudi nyumbani kwangu nikiwa na njaa, hakuna kesi ngumu kama kumfundisha Mwanaume kuandaa mke wake kabla ya tendo la ndoa.
Niliogopa baada ya kumuona Secretary Lui pamoja na bodyguard wa CEO wa hotel ya Burj Al.
"Nimekupigia sana simu usiku wa jana kwanini hukupokea" Secretary Lui aliongea
"Nilikuwa nimechoka sana sikusikia muito wa simu, kwanini mko hapa" Niliuliza
"Boss wetu anahitaji kupata breakfast nzuri kama ya jana naomba twende nyumbani kwake ukamuandalie, siku ya leo anaingia kazini mchana naomba tuwahi" Secretary Lui aliongea
Nilijikuta ni kikodoa macho kwa sababu watu hawa walikuwa kama wananiamrisha hivi na si kuniomba.
Nilishtukia tu na bebelewa juu juu na hili jitu linalojiita bodyguard Spark.
Nilitupiwa kwenye gari kisha safari ikaanza.
Dakika 25 hazikupita tulifika katika nyumba ya CEO wa Burj Al hoteli.
Nyumba yake ilikuwa na hadhi ya kasiri, nilipogeuka mkono wangu wa kushoto niliona kibao kimeandikwa "Mtaa wa Feisal" kuna watu wanapesa hadi mitaa inaitwa majina yao
Nilikaza moyo wangu, tukaingia kwa pamoja....moyo wangu ulilipuka baada ya kuona simba, twiga, swala na chui wakiwa wamefungiwa katika mabanda tofauti.
Sikuelewa hii ni nyumba au sehemu ya utalii
Mkojo kidogo ulipita kama masihala hivi baada ya Simba kuunguruma.
"Sura yako ni ngeni machoni kwake ndio maana kaunguruma" Bodyguard Spark aliongea
"Map*mbu yake!" Nilijisemea ndani ya moyo wangu
Ile napiga hatua, nilishtukia tu mpira umenigonga kichwani.
Niliangalia mbele nimuone mtu aliyenifanyia hivi, nilikutana macho na CEO wa hoteli ya Burj Al.
Hakuonesha kujali, jamaa hili lina kiburi na eti nimeletwa hapa kuandaa breakfast.
Nikiwa bado na hasira nilishtukia na pondwa na ndizi mgongoni, niligeuka nyuma kwa haraka nione mtu anayenifanyia hivi.
Nilishangaa baada ya kukutana na sokwe tena likinizomea.
"Hahahaaaahaha!" Feisal alicheka alionekana kufurahi
Nilishikwa na hasira niliokota ndizi iliyokuwa chini nikairusha ikagonga paji la uso wake
Itaendelea 💥
04
Bodyguard Spark alitaka kunipiga teke kwa kumponda na ndizi Boss wake
"Usisahau kama yuko hapa kuandaa breakfast ya Feisal, ukimvuruga utamlisha makalio yako" Secretary Lui aliongea kwa sauti ya chini
Bodyguard Spark ndio kupata akili alichukua mpira akamrushia Feisal, walianza kucheza kisha kisha Mimi na Secretary Lui tuliingia ndani.
Aisee nilijikuta ni kikodoa macho, kila sehemu niliyotazama ilikuwa ni nzuri sana.
"Karibu Madame, hili ndio jiko kuwa huru..." Secretary Lui aliongea
"Siwezi kuwa huru ni kama nahisi kila kitu hapa kinaniangalia.... naomba unisimamie mpaka nitakapo maliza kupika" Niliongea
"Usiwe na shaka, usisahau kama utalipwa hivyo pika kwa ustadi wa hali ya juu" Secretary Lui aliongea
Baada ya kusikia malipo nilizima kabisa simu yangu ni kaanza kupika.
Nikiwa napika huwa napenda kumfikiria sana Sultana wa kwenye Master of snacks 🥙 namna ya upishi wake huwa ni wa kipekee sana hata kama huna hamu ya kula ni lazima ule.
Secretary Lui alikuwa bega kwa bega na Mimi mpaka nilipomaliza, inaonekana wanamjali sana Boss wao.
1572
18:08
29.07.2025
Niliweka supu pamoja na chapati mezani, Feisal (Boss mwenyewe) alikaa akaanza kula.
Mie tena nilikaa zangu kwenye nikiwa nasubiria amalize kula nipatiwe malipo yangu
"Bodyguard Sparkkkkkk!" Feisal aliita kwa sauti ya juu, nilijikuta nikiogopa ndani ya moyo wangu japo Mimi si mtu wa kushtuka ila hili lisauti lilinishtua
"Yes CEO...." Spark aliongea baada ya kuja kama mshale
"Nimefurahishwa na hii breakfast....hakika nimefurahi sana" Fiesal aliongea
Ee bhana ee kwanini asiniambie hizi shukurani Mimi anamuambia Spark, nilijikuta nikicheka ndani ya moyo wangu
"Kwahiyo tunampa zawadi gani...." Spark alijiongelesha huku akijichekesha
"Kesho nina kikao na Wapishi wote katika hoteli yangu....tutamfanya kuwa Msemaji mkuu, pia nitampatia milioni 75 kwa kunifurahisha" Feisal aliongea
Nilijikuta nikishtuka niliposikia milioni 75, nilitaka nimtajie akaunti namba yangu lakini kwa kuwa wanazungumza kana kwamba Mimi sipo nilivunga pia.
Baada ya Feisal kumaliza kula alisepa hata bila kuniambia ahsante.
Nicheke mie, yaani Secretary Lui ndio kuja kunishukuru kwa niaba ya Boss wake.
"Nipatie akaunti namba yako nitakuingizia milioni 75, pia kesho nitakuja kukuchukua nyumbani kwako saa mbili kamili. Kutakuwa na kikao hotelini kwetu, Feisal kaona unafaa kuwa Msemaji mkuu"
Sikuwa na sababu ya kukataa, nimekuwa semaji la mtaa wa Igogo B kwenye kesi mbalimbali sishindwi kuwa main speaker kwenye kikao cha Wapishi wote kwenye hoteli ya Burj Al.
Nilimpatia Akaunti yangu kisha nikamsihi anisaidie kuondoka mahali hapa. Sikuwa tayari kufanyiwa fujo na Sokwe
Secretary Lui ni mtu mstaarabu sana kama angekuwa ni Mwanamke basi ningesema yeye ni Mama mjengo kwenye nyumba hii na Bodyguard Spark angekuwa ni Shangazi sababu ya muonekano wake wa kijeuri lakini huyu Feisal angekuwa ni Mwanamke mwenye kisirani cha mimba.
Ile tunakaribia kufika getini, tulisubirishwa kwanza. Bodyguard Spark alikuja kwa kukimbia
"Feisal anauliza unaitwa nani" Spark aliongea
"Naitwa Amina...." Niliongea
Spark alishika simu akarudisha mrejesho, sijui ilikuaje lakini alinipatia simu ni zungumze.
Nilichukua simu nikaweka sikioni mwangu.
"Amina...." Feisal aliniita
Sauti yake ilikuwa imetulia sana kama wale Watangazaji habari wa Kimataifa.
"Abeee...." Niliitika
"Nimefurahi kulifahamu jina lako Amina....uwe na siku njema" Feisal aliongea kisha akakata simu
Bodyguard Spark aliichukua simu yake, mie na Secretary Lui tuliendelea na safari ile nataka kufunguliwa geti, nililetewa simu tena na Spark
"Amina...." Feisal aliita
"Abeee ....." Niliitika, cha ajabu upande wa pili ulikaa kimya
Nilitaka kumrudishia simu Spark lakini aligoma alinisisitiza niendelee kuweka simu sikioni.
Dakika kama 20 hivi zilitembea bila Feisal kuongea.
"Amina...." Aliniita tena
"Abeee...." Niliitika
"Nitafurahi kama kesho utafika hotelini kwangu" Feisal aliongea kisha akakata simu.
Sikuwa tayari kupatiwa simu tena, kitendo cha Mlinzi tu kunifungulia geti niliondoka kwa kukimbia......
"Amina simama....." Niligeuka nyuma nikamshudia Bodyguard Spark akija kwa kukimbia huku mkononi akiwa ameshika simu
Itaendelea 💥
05
Nilisimama kujua ni kitu gani nataka kuambiwa
"Amina..." Feisal aliita
"Amina Mimi hapa niambie hicho kitu ulicho shindwa kuongea nikiwa nyumbani kwako...." Niliongea
"Tofauti nakupika ni kitu gani kingine unaweza kufanya kwa usahihi mkubwa..." Feisal aliuliza
"Tafuta muda kwa ajili yangu tutazungumza kuhusu hili...." Niliongea nikataka kurudisha simu
Bodyguard Spark alinipa ishara ya kujibu swali nililoulizwa na si kukwepa
"Nipo vizuri sana katika swala zima la kutatua migogoro, ukija mtaani kwetu nafahamika kama hakimu asiye na cheti. Pia nipo vizuri sana katika swala zima la sita kwa sita. Ikitokea nimekuonyesha ni lazima utanitafuta usiku na mchana. Kitumbua changu hakina tofauti na madawa ya kulevya" Niliongea
Feisal aliachia kicheko kikubwa, inaonekana maneno yangu yalimfurahisha sana.
"Sawa, uwe na siku njema...." Aliongea kisha akakata simu
"Sitarajii unifuate tena... nitakapo tega mgongo sitageuka nyuma" Nilimuambia Body guard Spark.
2555
18:08
29.07.2025
Hili jitu sijui lina kichaa au nini lilinibusu shavuni
"Ahsante kwa kumfanya CEO wangu achangamke namna hii..." Spark aliongea kisha akaondoka
Niliondoka pia, furaha yangu iliongezeka maradufu baada ya ujumbe wa shilingi milioni 75 kuingia kwenye simu yangu kutoka Burj Al hoteli.
Nilifika nyumbani kwangu nikiwa na furaha kubwa kupita maelezo, nilishangaa baada ya kukuta Sponsa wangu akikusanya vitu vyake alivyowahi kuninulia.
Sikutaka kuumia moyo, tena kwa uzuri kabisa nilimuitia bajaji imsaidie kubeba.
"Nenda tu, hata kama usingeniacha leo kesho ningekuacha. Nataka niwe kwenye mahusiano yanayoeleweka kuanzia sasa hivyo pita kule na Mimi nipite kule" Niliongea
Hili Sponsa ni jeuri sana, liliondoka bila kuniuliza chochote.
Niliachia sonyo kwa sababu kila gemu Mimi ndio nilikuwa mfungaji mwanzo mwisho sioni hasara kumpoteza
Sikutaka kupumzika hata kidogo, niliingia ndani nikabadili nguo zangu. Nilihitaji kwenda saluni kutengeneza nywele yangu.
Tangu nizaliwe sijawahi kuingia katika hoteli ya Burj Al.
Sikuona shida kutumia laki mbili kutengenezwa tu kichwani.
Mimi ni mjuzi wa kupangilia nguo, nilitafuta pamba zinazoendana na mandhari ya Hoteli. Si kila nguo inafaa kila mahali. Ili nionekane wa kipekee nilihitaji kufikiria vazi litakalo nifanya wa kishua.
Muda ulikimbia aisee, kulivyo pambazuka asubuhi tu Secretary Lui akiwa na gari la Burj Al hoteli alifika kunichukua.
Nilimshuhudia akiachia tabasamu bila shaka nilikuwa nimependeza kwa kiwango kikubwa.
Ingawa hakuongea chochote, kwa pamoja tulipanda gari.
Nilijikuta ni kitetemeka hasa nikifikiria eti leo naingia katika hoteli ya Burj Al.
"Relax, hii hoteli haina tofauti na migahawa midogo ya huko nje" Secretary Lui alinitia moyo
Nilijikuta nikicheka kwa sababu alikuwa ananitia moyo kimtindo.
Kwa pamoja tuliingia kwenye hotel ya Burj Al baada ya kufika.
Watu wote walinigeukia, pengine ni kwa sababu nimependeza sana au ni kwa sababu nimeongozana na Secretary Lui.
Sina kawaida ya kushangaa mtu mwenye jinsia kama yangu lakini Mwanamke aliyekuwa ana zungumza na Feisal alikuwa ni mrembo mfano wa katuni ya kishua.
"Huyo ni Mwanasheria wa Feisal, jina lake anaitwa Carolina. Amekaa sana uzunguni si mtu wa kupenda kuongea sana hivyo jitahidi kumpuuzia usioneshe shobo sana" Secretary Lui aliongea
"Oh Amina...." Feisal aliita kwa sauti kubwa baada ya kuniona.
Watu wote walinigeukia, nilijikuta nikishtuka.... macho ya watu yanatisha aisee
"Mimi hapa Feisal..." Niliongea kwa sauti kubwa pia, si kwa sababu nilikuwa najiamini hapana, sikuwa tayari kudondoka kwa sababu ya macho ya watu
Feisal alipiga hatua mpaka akanifikia sehemu niliyokuwa. Nilishangaa tu kanikumbatia.
Macho yangu yalikutana na ya Carolina, alinionesha tabasamu pana kana kwamba sisi ni marafiki.
Nilijikuta ni kimkodolea macho kwa namna alivyokuwa anavutia, uzuri wake ulipitiliza kiasi nilifumba macho.
"Amina...." Sauti ya Feisal ilinishtua ndio ni kafumbua macho.
"Amina jina lako zuri sana, si ajabu CEO wetu ana changanyikiwa...." Carolina aliongea
"Hahahaaaaa...." Feisal aliachia kicheko kikubwa huku akinigonga gonga begani. Watu wote walianza kucheka, inaonekana ni sheria CEO akicheka na Wafanyakazi wake ni lazima wacheke. Nilianza kucheka pia
💥FULL STORY WASAP👇👇
https://whatsapp.com/channel/0029VaoIWsl2v1Iu0ZtPgo2I
3558
18:08
29.07.2025
I LOVE HIM ❤️❤️1__5
SEHEMU YA 01
"Mama... Mwili unaniuma jana nimetembea umbali mrefu kwenda shuleni na kurudi sikupata hata lift ya baskel kila mtu alipanda na rafiki ake"
Alijilalamika moza huku akivuta shuka chakavu na kugeukia upande wa pili
"Mama ninunulie baskel"
"Moza upo lasita sasa hebu kamalizie mda uliobaki tutajua la kufanya ukienda sekondar japo sina uhakika"
Alijibu hadija au mama moza
"Haya haya...amka amka mihogo inapoa kule nimeibandika mda mrefu sinui kama haijaungua"
Pamoja na shida zote lakin mama moza alihakikisha kuwa moza anapata kifungua kinywa na anawah shule kila siku hata kama anatembea umbali mrefu lakin awe ameshiba maana kmaa mihogo tu analima pemben ya kajumba kao ka udongo.
"Lakin mama kwani baba angu yupo wap? Labda ningemuomba aninunulir baskel"
Moza alitupia swali kwa mama ake, ni swal anauliz akila siku ila hajawah kujibiwa.
"Kila siku mama nakuuliza hunipi majibu kila siku hunipi majibu mama baba yupo wap?"
"Moza, baba ako alifariki kitambo sana nashindwa kukujibu kwa sababu hata msiban sikuenda kulikuwa kipibd ambacho unazaliwa nae alifariki sasa unataka nifanyaje?"
Alijibu mama moza
"Namkumbuka sana baba ako mwanangu"
"Alafu mama, kama baba kafa ndugu wa baba wapo wap? Si wana uwezo? Au hawana helaa ya kuninunulia baskel?""
Aliuliza tena moza
"Unataka kuniudhi sasa moza, unataka kuniudh eeeh?"
Aliuliza hadija
"Nan kakufata shule kukujaza maneno? Wale mbwa wameanza kukufatilia na wewe?"
"Hakuna mtu mama"
Moza alijibu na kuwa mpole mmaa ake ni mkali sana.
"Mama mimi leo siog maana nimechelewa acha nivae niende shule hii wiki mwalimu wake mkali san"
'moza"
Hadija au mama moza aliita
"Kama kuna wapuuzi wanakufata huko shuleni waambie kabisa tena uwape habar zao kabisaaaa nitakufa na mtu sawa? Na habar za baba ako mwisho leo baba ako kafa"
"Kwa hyo Unamaanisha baba angu yupo hai?"
Moza aliuliza
"Unaogopa atanitafuta? Au mlikosana?"
"Hebu kwenda shule mjinga wewe unamuuliza nan hup upuuzi? Umekua?"
Alijibu hadija
"Harakaaa.... Na leo utembee tena akili ikukae sawa ili muda wa kuita baba baba ukose ukirudi ullae unanichosha tu mimi ndo babaa na.mimi ndo mama"
"Tunaulizwa Shule alafu wenzangu wamenunuliwa baskel na baba zao, mama ungeniamb..."
Moza hakumaliza mama ake aliokota kiatu na kumtupia akaokota na mwiko akamnyooshea
"Kavae uende shule mbuzi wewe, kawaambie mama ako ndo baba na ndo mama unaitwa mozaa bin gwama ubin wa mama angu ambae ndo bibi ako"
Alijibu mama moza
"Nenda shule nataka kufunga nyumba yangu niende zangu shamba unataka kuniuwa na presha? Baba baba angekuwa wa maana si ungemuona hapa"
"Sawa mama"
Moza alikubali yote
Moza aliondoka shule huku akiwa amechelewa sana anajua huko shule ni balaa mwalim wa zamu alikuwa mkali sana mwalimu kalugendo kama alivofahamika kwa kifup walimu wenzie walimwita luge alitingisha shule ipasavo kwa ushupavu wake wa kuchapa viboko wanaafunzi, zqmu yake alipangwa peke ake lakin aliimudu shule nzima.
Wiki yake ya zamu alikuwa anaagiza mzigo wa fito kila siku na zinaisha anaagiza zingine.
Wanafunzi weng walimuogopa mno, wanafunzi waliwah sana shuleni na walikuwa na nidhamu kubwa sana sana.
Moza alifika shuleni saa tatu kasoro akiwa ameloana majasho mwili mzima.
Anatetemeka haswa alipofika shulen na kumwona mwalim huyo kapigisha magoti wanafunzi wengne waliochelewa shule ila yeye alichelewa zaid anapokaaa na shule ni mbali mno na aanatembea kwenda na kurudi.
"Shikamoo mwalimu"
Alisalimia huku akipiga magoti na wenzake alijua wamechelewa tu
"We moza, piga magoti kule pembeni yan wewe unafika saa tatu? Kwenye zamu yangu? Labda sio kalugendo kaa mbali na hawa wamefika saa moja kasoro nne wewe umechelewa lisaa lizima"
Moza alishangaa sana maana huo ndo muda alioamka lakin wenzake wamepiga magoti tangu saa moja yeye alikuwa kitandan.
1589
00:32
05.08.2025
Aliokota fimbo alizotuma na kuwachapa sana wale waliochelewa kila mtu alitoka hapo anaugulia
Walichapwa had moza akaanza kulia pale pembeni yake kabla hajaguswa kaupepo ka kijijin na zile fimbo za asubh haikuwa rahiis kwensa kuandika darasan au kukaa kwenye kiti, wanafunzi wenzake weng walikuwa na baskel za kuwawaisha shule wa wasionazo walikuwa na marafiki hvo walipandishana wanne had watano baskel moja achilia mbali watoto wa walimu na wanaokaa karibu na shule ilikuwa rahis kwao kufika.
"Adhabu yenu mtasafisha mazingira ya hii shule kila siku, had zamu yangu iishe ndo mtaacha si mnapenda usingiz? Na ikifika saa moja na nusu muwe mmemaliza usafi na mmeingia madarasan ole wenu sasa"
Kalugendo aliagiza
"Sawa mwalimi"
Lile kundi la wanafunzi liliinukanna kutawanyika kwa spidi huku wakiugulia maumivu makal ya mwalim kaligendo
"Moza"
Mwalimu kalugendo alimgeukia moza
"Wewe kitanda chako ndo cha maana sana had unalala unasahau shule? Yan kinakubembeleza na ulivojaza funza kichwan ukabembelezeka"
"Mwalimu naomba nisameh"
Moza alijibu huku akijua zile fimbo zitamuishia mwilini maechelewa kuliko wenzake.
"Nafikiria nikurudishe kwenu ukalete mzazi aje aseme nini kimekuchelewesha huwez kuja shule saa tatu"
Kalugendo alijibu huku akichagua fimbo nzuri zaid
"Hebu sogea hapa na sket lako hilo kama linetafunwa na ng'ombe wa kimasai"
Moza alisogea na kuanza kushushiwa bakora za kutosha pale uwanjani. Bakora ya kwanza tu moza alichanganyikiwaa hakuweza kukinganmkono tena.
Kalugendo hakuwa anahesabu alimtandika tu na kumtandika had aliporidhika na alimchapa popote alipoona panafaa.
Moza alibaki analia ni yeye peke ake alikuwa amechelewa zaid ya wenzake ni kwel alifika hapo saa tatu kasoro.
"Nikupe adhabu gan?"
Aliulizwa
"Nifagie uwanja"
Alijibu moza huku akitetemeka kalugendo alimchapa had fimbo ilibaki kipisi.
"Yan wewe uchelewe alafi unifagilishe uwanja na waliowah? Unaakili kweli? Hebu acha upumbavu, wewe utadeki vyoo vyote vya wavulana, vya wasichana na vya walimu had nimalize zamu sawa?"
Kaligendo aliuliza
"Na ole wako uchelewe tena na ikifika saa moja na nusu kesho uwe mstarin na wenzako""
Moza alihisi kuchanganyikiwa mno.
Kazi ya kudeki vyoo ilikuwa kubwa kwake kutokana na umbali anaokaa, pia wingi wa vyoo vya wanafunzi tatu vyoo vilikuwa vichafu mno haswa wanaojisaidia pemben kwa haja zote nne maji ya kudekia yalikuwa yanapatikana mbali na hapo shuleni alafu adeki peke ake ilikuwa ni mgogoro.
Alitaman kuacha hata shulen lakin hakuwa na namna,angemuambiajd mama ake na vile alivomkali? Angemwambiaje mwalimu adhabu ni kubwa jinsi mwalimu alivo mkali alibaki kukaa kimya na kuumia Moyon.
"Mwalimu naomba nianze kesho, nimechelewa sana masomo"
Moza alilalamika huku analia
"Nitadeki kesho"
"Kungekuwa na umuhimu kusoma ungewah shule, kadeki ndo uingie darasan, si unaona wenzako wanafagia? Unabishana?"
Aliuliza kalugendo
"Hapana'
Moza alijibu na kwenda stoo kuangalia kama kuna ndoo lakin zilikuwa zimepasuka alibahatika kupata ndoo moja tu nayo ilikuwa imekatika kwa juu hvo hapakuwa nauwezekano wa kubeba maji meng kwa wakat mmoja hapakuwa na vyombo.
Moza alihisi kuchanganyikiwa aliona shule ni chungu katika wiki ya kalugendo ndivo inavokuwa ila yeye kuchelewa zaid ilikuwa ni balaa.
Alikaa chini na kuanza kulia, alilia kwa uchungu sana aliwaza meng pamoja na kupata shida kufika shule lakin alikutana na adhabu, fimbo n adarasan haingii.
"Baba upo wap!!!! Baba mimi ungeninunulia baskeli tu leo nisingepata adhabu"
Moza aliongea kwa uchungu
"Nadeki vyooo vyote hv, baba...umekufa? Mbna ulikufa kabla hujaninunulia baskel?"
"Moza unataka nini kwangu?"
Kalugendo alisimama mliman kumtazama moza kwa bonden alipokaa karibu n avyoo vya shule.
"Leo hutaenda kwenu bila kumaliza hvyo vyoo na wiki zote mbili utadeki chunga sana ntachukua zamu ya mwezi ili mnyooke noana kabisa mnafanya ujinga"
Moza aliinuka na kutelemka bondeni kuufata mto kwa ajili yakichota maji akadeki vyoo saut ya kalugendo ilikuwa kali mno angemuua na fimbo kama angekaidi.
1532
00:32
05.08.2025
"Kichwa kibaya na bado mvivu nasema hv wavivu wote mtanyooka safar hii kama mnacheza chezen na walimu wengne sio hii namba ya kalugendo"
Alijibu kalugendo huku moza aliteremka kwenda mtoni kwa kasi sana
I love him ❤️❤️2
Hali ilikuwa mbaya sana, moza alishuka mtoni pke ake na kuchota maji akaanza kudeki vyoo, vyoo vya wanafunzi kama ilivo kawaida ni vichafu mno mikojo inakuwa imejaa korido nzima .
Mbali na wengne kumkuta anadeki bado kuna wale walioingia kuvitumia wakat wamemkuta hajamaliza usafi hvo ilimlazimu kurudia ili mwalim kalugendo akute vyoo visafi.
Alipiga ruti za mtoni na kwenye vyoo had mda wa masomo ulipoisha ndipo alipomaliza kudeki alikuwa amechoka sana, bado mwalimu alimuandama kwenda kuvikagua kama vimetakata au la ilikuwa siku ngumu sana kwake.
"Kesho nikute vyoo vimedekiwa vizuri tena kesho kupindi changi ni cha kwanza ole wako uchelewe kudeki na ole wako ukose kipind kama vitanda vyetu vinakunguni basi kungun zitahmaia kwako utawah tu kuamka mbna"
Kaligendo alichimba mkwara mkali.
"Sawa mwalimu"
Moza alijibu na kuanza kuondoka
Wanafunzi wangi walishatawanyika eneo hilo la shule mda wa vipindi uliisha ila yeye alideki vyoo siku nzima. Yanni kama siku hyo alienda kudek vyoo vya shule tu na si kufata masomo.
Alitembea njia nzima analia huku anarudi nyumbani, moyo ulimuuma sana adhabu ya viboko aliyopewa ilimtosha na ilikuwa kubwa ila kudeki vyoo na maji yapo mbali ilikuwa kubwa zaid tena vyoo vya kike na vya kiume achilia mbali vya walim ambavyo aangalau vilikuwa visafi.
Alifika nyumbani giza lilishaanza kuingia kabisa maana shule na kwao ni mbali mno.
"Kwanini umechelewa, mbna unapenda kunipa hofu we mtoto? Umepata mwanaume?"
Aliuliza mama ake kwa mshangao
"Nimechelewa shule mama mwalimu alichonifanya mimi"
Moza alijibu huku akikaa chini kuendelea kulia
"Mama naacha shule"
"Moza, mozaa...."
Mama ake aliwaka
"Umepata bwana eeh? Amekudanganya si ndio? Alisema atakuoa?"
"Mama nimechelewa shule nimepigwa ona mikono ona mikono mama mwalim anapiga kama anataka kuua mama"
Moza alionesha mikono yake
"Na bado nimepewa adhabu ya kudeki vyooo wiki mbili zote maji yapo mbali leo sijaingia darasan sijasoma mimi"
"Et nini?"
Mama moza alishangaa
"Sijaingia darasan mama nimedeki choo tu asbh had jion hpaa mwili wote unauma mama, mini siend had mwalim amalize zamu yake"
Alijibu huku analia alibadilisha kauli ya kuacha anajua mama ake ni kichaa
"Mwalimu hanipendi mimi"
"Weww nani? Shule nzima wewe ni nan uchukiwe? Moza unafurahia umasikin? Hutaki shule ili?"
Mama moza aliuliza
"Nitolee uvivu wako hapa, kavue hzo nguo uoshe vyombo na ole wako uache shule na kesho lazima uende, si nilisema uende shule ukaanza upuuzi wa baba baba"
"Mama laki..."
Moza alishangaa mama ake hayupo upande wake hata kidogo
"Kelele"
Alijibu huku akitaka kumrushia mwiko aliokuwa anasongea ugali wa usiku
"Sibishani mara mbili hapa ngedere wewe kavie hzo sare haraka uoshe vyombo"
Moza aliinuka na kuingia ndani, alichoka mno mwili haukuwa na ushirikiano alibadilisha nguo na kuingia kuosha vyombo vya jana yake.
Shughuli za nyumbani ziliisha saa nne usiku ndipo alipopanda kitandani kujipumzisha mwili ulikuwa hauna ushirikiano kabisa.
Pamoja na kuwa wanaishi wawili tu lakin kazi zilikuwa nying mara nying mama ake alishinda shamba na usiku alitoka moza hakuwa anajua mama ake anaenda wap, alikuwa anamwona anatoka tu na hajui anarudi saa ngap ila asbh anamwona.
Alfajiri moza aliamka mapema kuliko kawaida alijiandaa na kuondoka kwenda shule, siku hii hakusubri chai wala hakungoja chochote kile alijua kalugendo angemuua alivaa haraka haraka hataa kagiza kalikuwa hakajaisha la yeye aliondoka bila hata kujua saa ngap.
Alitembea njian huku anakimbia palikuwa hapajapambazuka bado alifika shule barid kimempiga ila hakujali alisombelea maji na kudeki vyoo haraka haraka saa kumi na mbili na nusu alikuwa ameshamaliza kudek vyoo vyote kaabla wanafunzi hawahafika wakaanza kuvitumia.
1707
00:32
05.08.2025
Kalugendo alishangaa sana, moza aliwah kuliko kawaida yake.
"Kumbe kuwah unajua? Leo ungelia kikwenu nilidhan unalala angan kumbr unalalia kitanda? Bas utaamka mapema kila siku"
Alimwambia huku akikusanya fito kwa ajili ya wachelewaji.
Siku hii moza alisoma na kuandika walichosoma wenzake jana yake haraka haraka laijua angekutanaa na kesi ya pili ya kutoandika darasan.
Siku ilienda vema kabisa hakuwa na ugomv na mwalimu wala mtu yoyote shuleni hapo na hakubahatika kupata fimbo za mwalim kalugendo au luge kama walivomfupisha.
Siku hii mpya Bahat ilikuwa mbaya zaid moza alikuwa amechoka mno hvo alilala zaid alifika shuleni saa mbili asubhi na kumkuta kalugendo darasani ameshaingia na vyoo hajadeki.
"Moza moza moza"
Alimwita huku akifata fimbo zake na kumsogelea pale mlangoni
"Shika vidole vya miguuni"
"Mwalimu naomba nichape mkonon tafadhali"
Moza laijibu huku ananyoosha mkono
"Mwalim nakaa mbali"
"Mbaki mbinguni? Shika vidole vya miguuni huwez kunipaangia pa kukupiga ngedere wewe"
Mwalimu kalugendo alijibu.
Moza aliinama, mwalimu kalugendo alishika fimbo vizuri na kushushaa fimbo moja tu liyotua ilikatika moza laikimbia nje na kuacha begi lake mle darasani ni kama alichanganyikiwa
"Nisamehe mwalim nisamehe"
Alionge ahuku anatoka nje.
"Oookh unakimbia? Haya nenda nisikuone hapa na kipindi changu nimekufukuza kuanzia leo"
Kalugendo aliokota begi la moza na kumrushia moza huko nje ila moza hakuweza hata kuliokota ile fimbo iliingia had kwenye mifupa utadhan mtu kamchapa kwenye mfupa.
Alikaa chini ya mti na.kulia sana, alilia mno alitazama vile vibaakel na wenzake darasan aliumia mno.
"Kwan baba angu kafa kweli? Ndugu wapo wap?"
Alijiuliza moza alitaman kuwajua ndugu wa baaba ake akaombe msaada wa baskeli hoyo ndo ilikuwaa kiu ya moyo wake.
Mwalimu kaligendo alitoka darasan na kumkuta moza amekaa chini ya mti analia bado kipindi cha masaa mawili kiliisha moza alikuwa hajainuka analia tu.
"Umedeki vyoo?"
Aliuliza kalugendo huku akimftaa moza na fimbo.
"Mwalimu naomba nisamehe"
Alilalamika moza huku analia
"Mwalimu mimi nakaa mbali"
"Wapi? Wap?"
Kalugendo laiuliza
"Mimi nakaa kisogota kwa mbele huko wewe unavuka manyama wewe? Unavuka manyama au kisogota?"
"Hapana"
Moza alijibu
"Kumbe unakaa karibu kabisa nasema hv moza utawah tu shule yan utawah tu utaamka kila siku utawah na nitakufatilia mbna wenzako wanawah? Baba ako si akununulie baskeli au huna wazaz?"
Alijibu kaligendo
"Kadeki vyoo haraka miguu kama banio la ugali"
Moza alintazama yule mwalimu alihisi kweli mama ake angemweleza baba ake alipo angenunulia baskeli. Aliinuka haraka pale chini aliogopa kupigwa tenaa alibeba begi lake na kwenda kudeki vyoo kama ilivo ratiba yake na shida maji yapo mbali.
Hali ilikuwa ngumu sana kwake, maisha ya shule yalikuwa magumu mno haswa kwa mwalimu kalugendo wiki yake ilikuwa ngumu zaid mwalim ni mkali na hasikilizi mtu wa aina yoyote ile.
Alibeba ndoo yake kipande naa kwenda kuchota maji ya kudekia vyoo sasa.
"Moza moza"
Akiwa mtoni alisikia mtu anamwita na kumgusa, moza alishtuka sana hakujua kama kuna mtu angemgusa huko mtoni mshtuko alijikuta anatumbukia mtoni mzima mzima na sare zake za shule.
"Sakina"
Moza alihema kaa kasi huku akiinuka ameloana tepetepe
"Mbna unanishtua hvo, ntakufa mwenzako unaona nimeloanaa"
"Mbna unaogopa, nakuon akila siku lazima uchote maji huku vip?
Aliuliza sakina
"Umepewa adhabu na hiyo mpuuzi? Au maji ya nini"
"Mpuuzi gan?"
Moza alishangaa wanafunzi kumwita mwalimu mpuuzi lilikuwa geni kwake.
"Si kalugendo"
Sakina alijibu
"Au sio klaugendo alokupa adhabu?"
"Sina hata chankusema amenipiga kidogo anivunje mgongo hapa nna adhabu ya kudeki choo kwa wiki mbili"
Moza alijibu
"Acha niwah had nimalize kudeki ntakauka"
"Acha ujinga wewe kwan huwazi? Umekuja kudeki vyoo? Moza changamsha akili"
Sakina alimwambia
"Wenzako tukichelewa tunachili kichakan had mda wa mapumziko ndo tunaingia daraan wewe unashindaa nini?"
"Mmmh mama angu akijua?"
Moza aliogopa sana
"Acha nikadeki vyoo, sakina mama angu mkali sana ntajua cha kufanya lakin sio kujificha huku"
3012
00:32
05.08.2025
"We mpuuzi kweli kama huyo maalimu, mi nilitaka nikusaidie tu bas lakin kama ni hivo ni sawa utadki mikojo ya watu had upate UTI ya kichwan yan maji yapo mbali bado ukadeki mavyoo peke ako mimi siwez"
Aliongea kwa dharau na kurudi kichakani.
Moza alisombelea maji na kudeki vyoo had muda wa watu kurejea nyumbani na yeye alirejea bila kusoma tena aliishia kudeki vyoo tu siku hyo.
Alibaki kushangaa sana hata yeye hakuelewa kwanini imekuwa hvo.
Jion Akiwa anakanyaga na mguu kurudi nyumbani alisimama kijana mmoja na baskeli karibu yake
"Pole moza"
Aliongea kijana huyo n akumtazama moza usoni.
"Nasikia kalugendo anakuandama sana leo alitaka kukuvunja"
"Asante nimeshapoa mambo"
Alisalimia moza akitarajia lifti ya baskel kwa kijana huyo manaa alikuwa na baskeli
"Poa, baskel yangu haina kiti cha abiria ningekubeba najua umechoka"
Kijana huyo alishuka kwenye baskeli yake na kumtazama moza
"Naitwa koya"
"Nakujua"
Moza alijibu
"Nan asiemjua koya kiranja mkuu wa shule nakujua koya"
"Aakh nilitaka kujitambulisha usikie kutoka kwangu mwenyew najua weng wananijua ila mimi siwajui"
Koya alijibu
"Panda kaa kwenye bomba ila pale mliman itabd tutembee maana sitoweza kuendesha"
"Asante sana koya"
Moza alifurah sana alipanda baskel mdogo mdogo koya aliiendesha huku akitabasamu
"Mungu akibariki koya yan sijui ningefika nyumban saa ngap"
"Moza sisi ni binadamu isitoshe ni wanafunzi ni muhimu kusaidiana katika safar ya masomo ili kila mtu afike"
Alijibu koya
"Unakaa wap?"
"Mimi nakaa manyama"
Alijibu moza
"Na wewe?"
"Mimi sifiki manyama nakaa nyuma ila usijali nitakupeleka had kwenu"
Alijbu koya
"Kama hutojali uwe unaamka mapema sana nakuja kukufata maana kalugendo atakuuwa"
"Kweli koya"
Moza hakuamin maishan mwake kupata msaada wa ghafla et koya awe anakuja kumfata na kupeleka shuleni na wakat hafiki manyama kwao nyuma kabisa aliona mungu ameshusha msaana
"Mimi nisaidie wiki ya mwalim kalugendo tu zingine ntatembea usijichoshe"
"Wala usijali moza, unajua mimi nataka thawabu kwa mungu tu ila nataman uishi kwa aman kama sisi utadeki vyoo kila siku jaman?"
Aliuliza koya
"Umekuja kusoma sio kudeki vyoo"
Moza alijikuta anafurah sana hata lile wazo la sakina et akichelewa awe anakaa kichakani had mda wa kupumzika alilisahau.
Ratiba ilibadilika alikuwa anawah sana shule kabla ya mwalimu akiwa na koya, anamsaidia watu wanachota maji na wanadeki vyoo haraka harak kabla ya mwalim kuja.
Aliwah shule wiki zite mbili na kumaliza adhabu yake ya kudeki vyoo kwa ushirikiano wa wanafunzi wengne.
Maisha ya moza yalibadilika kias alikuwa anaenda shule kwa wakat na kurudi bila kuchoka hata mama ake hakupata malalamiko ya kuulizwa baba yupo wap maana ile hamu ya baskel alipata baskel ya msaada kuletwa na kufaatwa kama bosi vile.
Koya na moza waliiva urafiki na ukaribu wao uliongezeka maraduf had kila mtu alihisi kama moza na koya wana uhusiano wa mapenzi lakin haikuwa hvo walikuwaa marafiki wa kawaida ty.
Koya hakuwah kumtamkia moza et nakupenda sijui upuuzi gan hajawah kutamka ila alikuwa anambeba kama mdogo wake na kumfata asubuhi.
Tetesi za mahusiano ya kimapenzi kati ya moza na koya zilifika kwa mwalimu wa nidhamu kalugendo.
Laishangaa sana hakuamin kama kaka mkuu wa shule ndo anaongoza kuwa na mahusiano ya kimapenzi tena ya wazi shuleni.
"Koya huyu huy?"
Alibaki kuuliza
"Kaka mkuu?"
"Ndio mwalimu anambeba moza tena pale mbele kwenye baskel na jion moza anamsubr wanarudi wote hata moza atooke amechelewa koya anamngoja"
Mbea alipeleka habar moto moto kwa mwalim
"Nitachunguza, nitajua kila kitu kumbe koya hana akili? Yule moza kampa nini koy? Haf anamharibu kaka mkuu?"
Laiuliza kalugendo
"Hatujui hata sisi tunaona ukaribu unazidi mwalimu wewe angalia asbuh na.jion utaona moza na koya wapo pamoja kama sio baskel basi wamebebeana mabegi"
Mbea alizid kutoa umbea
"Tena koya ndo anabeba begi la moza"
JIUNGE WHATSAPP 👇👇
https://whatsapp.com/channel/0029VaoIWsl2v1Iu0ZtPgo2I
4463
00:32
05.08.2025
THE GAME OF LOVE❤️
IPO WHATSAPP 👇👇
https://whatsapp.com/channel/0029VaoIWsl2v1Iu0ZtPgo2I
2860
08:58
10.08.2025
imageImage preview is unavailable
GENERAL DAVID
IPO WHATSAPP 👇👇
https://whatsapp.com/channel/0029VaoIWsl2v1Iu0ZtPgo2I
1004
18:38
19.08.2025
close
Specials
BETTING AND GAMBLING

Channels
13
239K
lock_outline
CPM
lock_outline$$ 1 286.74
$$ 1 158.07
-10%
Reviews channel
keyboard_arrow_down
- Added: Newest first
- Added: Oldest first
- Rating: High to low
- Rating: Low to high
5.0
1 reviews over 6 months
Excellent (100%) In the last 6 months
c
**ffeenold@******.io
On the service since June 2022
21.05.202520:36
5
Everything is fine. Thank you!
Show more
New items
Channel statistics
Rating
22.6
Rating reviews
5.0
Сhannel Rating
3
Subscribers:
21.8K
APV
lock_outline
ER
2.6%
Posts per day:
3.0
CPM
lock_outlineSelected
0
channels for:$0.00
Subscribers:
0
Views:
lock_outline
Add to CartBuy for:$0.00
Комментарий